Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika Bi. Ann Therese NDONG-JATTA (kushoto) na Mwakilishi Mpya wa UNESCO nchini Tanzania Bw. Tirsa A.S Dos Santos (kulia) ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Tanzania Inazalisha Chakula Kingi Cha Kutosha – MAKAMU WA RAIS

  • Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo kwa nyakati tofauti na Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni, Balozi wa Falme za Kiarabu nchini Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi pamoja na Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika Bi. Ann Therese NDONG-JATTA ambaye alimtambulisha Mwakilishi mpya wa UNESCO nchini Tanzania Bw. Tirso A.S Dos Santos.
  • Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni amesema nchi yake itaendelea kushirikiana na kuisaidia Tanzania katika masuala mbalimbali hususani kwenye sekta ya Elimu ambayo kuna mikataba na Tanzania na kwenye sekta Afya kupitia taasisi isiyo ya kiserikali ya CUAMM.
MAKAMU WA RAIS
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika Bi. Ann Therese NDONG-JATTA pamoja na Mwakilishi Mpya wa UNESCO nchini Tanzania Bw. Tirsa A.S Dos Santos ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • Balozi huyo amesisitiza kuwa Italia itaendelea kusaidia yale mambo ambayo nchi imeyapa kipaumbele.
  • Balozi Mengoni ameipongeza Serikali kwa kuanzisha mfumo wa visa na vibali vya ukaazi vya kielektroniki ambao utarahisisha huduma ya upatikanaji wa visa.
  • Makamu wa Rais amemueleza Balozi huyo kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Italia na kuiomba nchi hiyo kupitia taasisi isiyo ya Kiserikali ya CUAMM kutoa elimu ya lishe bora kwa watoto.
MAKAMU-4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika Bi. Ann Therese NDONG-JATTA ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • “Tanzania inazalisha chakula kingi sana ukitembea huko vijijini watu wanalima sana lakini lishe bora kwa watoto bado ni tatizo, kunahitajika elimu zaidi” alisema Makamu wa Rais.
  • Makamu wa Rais pia alikutana na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu Nchini Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi ambaye alimueleza Makamu wa Rais nia ya kujenga Ofisi za Ubalozi mdogo Zanzibar mwakani.
  • Pamoja na mambo mengine Balozi huyo amewataka Watanzania kuchangamkia fursa katika maonyesho ya kimataifa ya Expo 2020 yatakayofanyika Dubai.
  • Kwa upande wake Makamu wa Rais alimueleza Balozi huyo kuwa Tanzania inashukuru kwa ushirikiano mzuri na itaendelea kutoa ushirikiano katika nyanja mbali mbali.
  • Mwisho Makamu wa Rais alikutana na Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika Bi. Ann Therese NDONG-JATTA ambaye alimtambulisha Mwakilishi mpya wa UNESCO nchini Tanzania Bw. Tirso A.S Dos Santos.
MAKU
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika Bi. Ann Therese NDONG-JATTA ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • Mkurugenzi huyo wa UNESCO Kanda ya Afrika alimueleza Makamu wa Rais mafanikio ambayo UNESCO wameyapata kupitia mradi wake wa kutoa elimu kwa maeneo yasiyofikika kwa mfumo wa kidijitali, elimu kwa watoto wa kike, radio jamii pamoja na huduma ya telemedicine ambapo mgojwa anaweza kupata huduma kwa simu.
  • “UNESCO imeendelea kutoa semina na elimu mbali mbali hasa katika Nyanja ya habari ili kuhakikisha watoaji habari wanatoa habari sahihi” alisema Mkurugenzi huyo.
  • Kwa upande wake Makamu wa Rais alimpongeza Mwakilishi mpya wa UNESCO nchini na kumkaribisha, pia ameipongeza UNESCO kwa ujumla kwa kazi nzuri wanayoifanya Tanzania.
  • “Ningeomba radio jamii zitoe elimu zaidi katika kampeni za masula ya ukeketaji, lishe bora kwa watoto na afya ya mama na mtoto”alisema Makamu wa Rais.
Ad

Unaweza kuangalia pia

SERIKALI KUENDELEA KUCHUKUA HATUA KWA WAZALISHAJI NA WASAMBAZAJI WA MIFUKO ISIYOKIDHI VIWANGO – WAZIRI ZUNGU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *