SERIKALI KULIPA MAFAO YA WALIMU 2631 KABLA YA MWEZI AGOSTI, 2020

Rais Dkt. John Magufuli amesemea kuwa Serikali italipa mafao ya walimu kabla ya mwezi wa Agosti mwaka huu ambapo walimu wanaodai mafao yao ni 2631, amesema hayo katika mkutano wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) uliofanyika mjini Dodoma

“kwa taarifa za jana kutoka mfuko wa PSSSF umepokoea na kulipa trilioni 1.2 kwa walimu wastaafu 15,029 kati ya mwezi Agosti 2018 hadi tarehe 3 Juni 2020 madai yaliyobaki ya walimu 2631 wanaodai bilioni 215 napenda kuwa ahidi hapa kabla ya mwezi Agosti haujafika hawa wote watakuwa wamelipwa fedha zao” Rais Magufuli

Ad

Akizungumzia vipaumbele vya serikali katika sekta ya elimu ni Rais Magufuli amesema kuwa sekta ya elimu inaendelea kuboreshwa na ndio sababu Serikali imebeba jukumu la kugharamia masomo ya shule za msingi na sekondari ambapo toka Desemba 2015 – februari 2020 serikali imetumia trlioni 1.01 kugharamia masomo wanafunzi na kuwaondolea wazazi jukumu hilo.

Aidha, amesema kuwa serikali imeongeza idadi ya shule za msingi kutoka 16,899 mwaka 2015 hadi kufika 17,804 mwaka 2020, kwa upande wa shule za sekondari amesema kuwa idadi ya shule zimeongezeka kutoka 4,708 mwaka 2015 hadi 5,330 mwaka 2020.

Kwa upande wa shule kongwe za sekondari amesema kuwa shule 73 zimekarabatiwa kati ya shule kongwe 89, na kuongeza kuwa mabweni 253 yamejengwa na kuongeza vyumba za mahabara 227 na kupeleka vifaa 2,956 katika maabara hizo.

Rais Magufuli amesema kuwa Serikali pia imeongeza idadi ya madawati kutoka milioni 3 hadi kufikia milioni 8 na hivyo kusaidia kumaliza tatizo la madawati katika shule.

Akizungumzia upande wa vyuo amesema kuwa vyuo 18 vya ualimu vimekarabatiwa na ujenzi wa vyuo viwili vipya vya Mrutuguru na kabaga vimejengwa

Aidha, Amesema Serikali imepeleka komputa 1,550 katika vyuo vyote 35 kwa lengo la kuboresha ufundishaji katika upande wa tehema, Rais Magufuli ameongeza kuwa serikali imeongeza vyuo vya VETA kutoka 672 hadi kufikia 712 mwaka 2020 na kufanya ukarabati na kuboresha vifaa vya kufundishia katika vyuo 54 vya Maendeo ya Wananchi (FDC)

Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS SAMIA ATEMBELEA RUKWA.. AANGAZIA AFYA, ELIMU, KILIMO NA MIUNDOMBINU KWA MIRADI YA MAENDELEO.

Katika ziara ya Rais Samia siku ya leo iliangazia kwenye sekta ya Afya, Elimu, Kilimo …

4 Maoni

  1. You actually make it seem so easy along with your
    presentation but I to find this matter to be really one thing that I
    feel I would never understand. It sort of feels too complicated and extremely large for me.

    I am taking a look ahead to your next publish, I will try to
    get the hold of it! Escape rooms hub

  2. You have observed very interesting points! ps nice website.!

  3. Oh my goodness! Impressive article dude! Thank you so much, However I am going through issues with your RSS. I don’t know the reason why I can’t subscribe to it. Is there anyone else having identical RSS issues? Anybody who knows the solution will you kindly respond? Thanks!!

  4. Can I simply say what a comfort to find somebody who genuinely knows what they’re discussing on the net. You certainly understand how to bring a problem to light and make it important. A lot more people really need to check this out and understand this side of your story. I was surprised that you are not more popular because you surely possess the gift.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *