MCHIMBAJI ALIYEPATA MADINI YA TANZANITE YENYE THAMANI YA SH. BILIONI 7.8 AMPONGEZWA NA RAIS MAGUFULI

Mchimbaji Bw. Saniniu Laizer (kushoto) akiwa amebeba madini ya Tanzanite amabyo yana jumla ya kilo 15 ambapo jiwe moja lina kilo 9. 2 la thamani ya bilioni 4.5 na lingine kilo 5.8 lenye thamani ya shilingi ya bilioni 3.3 wakati wa tukio la kuuza madini hayo kwa Serikali
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashantu Kijaji  akionyesha madini ya Tanzanite ambayo yamenunuliwa na Serikali kwa thamani ya Shilingi bilioni 7.8 kutoka kwa mchimbaji Bw. Saniniu Laizer
Waziri wa Madini Doto Biteko akizungumza wakati wa kukunua Madini ya Tanzanite yenye thamani ya shilingi bilioni 7.8 kutoka kwa mchimbaji Bw. Saniniu Laizer tukio lililofanyika Wilayani Simajiro Mkoani Manyara.

Rais Dkt. John Magufuli amempongeza mchimbaji mdogo madini Bw. Saniniu Laizer kwa kupata mawe mawili ya Tanzanite yenye thamani ya shilingi bilioni 7.8 ambayo ameyauza kwa serikali.

Rais Dkt. Magufuli ametoa pongezi hizo wakati akizungumza kwa njia ya simu na Waziri wa Madini, Doto Biteko ambaye ameongoza zoezi la serikali katika ununuzi wa madini hayo ambayo moja lina kilo 9.2 lenye thamani ya shilingi bilioni 4.5 na lingine likiwa na kilo 5.8 lenye thamani ya shilingi bilioni 3.3.

Ad

“Na hii ndio faida ya wachimbaji wadogo wadogo na hii ni kudhihirisha kwamba Tanzania sisi ni matajiri kwahiyo nawapongeza sana viongozi, nakupongeza sana wewe Waziri wa Madini, Wizara ya Fedha nampongeza Gavana ,nawapongeza viongozi wa mkoa wa Manyara, Kilimanjaro pamoja Arusha lakini nawapongeza sana wananchi wa Simanjiro kwa kazi nzuri wanazofanya za kujitajirisha” Amesema Rais Magufuli

Rais Magufuli amesema kuwa Tanzanite hiyo ni kubwa na haijawahi kupatikana maeneo mengine na hivyo kupongeza hatua ya serikali kuamua kununua madini hayo.

Tukio hilo la ununuzi wa Madini hayo limefanyika Wilaya ya Simajiro mkoani Manyara katika kituo cha kuuzia madini, ambapo limehudhuriwa na Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Ashantu Kijaji, Gavana wa Benki Kuu Prof Florens Luoga, Mbunge wa Jimbo la Simanjiro James Millya, Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanajro Anna Mghwira na viongozi mbalimbali katika Sekta ya Madini.

Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS SAMIA ATEMBELEA RUKWA.. AANGAZIA AFYA, ELIMU, KILIMO NA MIUNDOMBINU KWA MIRADI YA MAENDELEO.

Katika ziara ya Rais Samia siku ya leo iliangazia kwenye sekta ya Afya, Elimu, Kilimo …

152 Maoni

  1. Добрый день!
    Мы можем предложить документы ВУЗов, расположенных в любом регионе Российской Федерации. Можно приобрести качественно сделанный диплом от любого заведения, за любой год, указав актуальную специальность и хорошие оценки за все дисциплины. Дипломы и аттестаты печатаются на бумаге самого высшего качества. Это позволяет делать настоящие дипломы, не отличимые от оригинала. Документы будут заверены необходимыми печатями и подписями.
    datasphere.ru/club/user/12/blog/4373/

  2. Здравствуйте!
    Покупка диплома о среднем полном образовании: как избежать мошенничества?
    mockwacom.getbb.ru/viewtopic.php?f=11&t=1728
    Поможем вам всегда!.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *