Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Agosti, 2020 amekagua magari yaliyotaifishwa baada ya kuhusika katika matukio ya uhujumu uchumi, na kisha kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani Jijini Dodoma.
![](https://matokeochanya.co.tz/wp-content/uploads/2020/08/c2_1-1024x683.jpg)
baada ya kuhusika katika matukio mbalimbali ya uhujumu yakiwa
yamehifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma
yaliyokaguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli leo Jumanne Agosti 25, 2020
Idadi ya magari hayo ni 130 yakiwemo makubwa na madogo yalikamatwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini, kisha wahusika kufikishwa Mahakamani na Mahakama kutoa uamuzi wa kuyataifisha.
![](https://matokeochanya.co.tz/wp-content/uploads/2020/08/c3_1-1024x683.jpg)
Pombe Magufuli akikagua magari makubwa na madogo 130 yaliyotaifishwa
baada ya kuhusika katika matukio mbalimbali ya uhujumu yaliyohifadhiwa
kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma leo Jumanne Agosti 25, 2020
Akizungumza baada ya kuyakagua, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Jeshi la Polisi na wote waliohusika kuwakamata waliokuwa wanajihusisha na vitendo hivyo (ikiwemo biashara haramu ya meno ya tembo) na ameagiza magari hayo yagawanywe katika taasisi mbalimbali za Serikali ili yatumike kuendesha shughuli za kuwahudumia wananchi na kuzalisha mali.
![](https://matokeochanya.co.tz/wp-content/uploads/2020/08/c4_1-1024x683.jpg)
Pombe Magufuli akikagua magari makubwa na madogo 130 yaliyotaifishwa
baada ya kuhusika katika matukio mbalimbali ya uhujumu yaliyohifadhiwa
kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma leo Jumanne Agosti 25, 2020
Mhe. Rais Magufuli pia amewapongeza wananchi waliojitokeza kutoa taarifa zilizosaidia kukamatwa kwa watu waliokuwa wanafanya uhalifu kwa kutumia magari hayo na amewaomba waendelee kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola ili kukomesha vitendo hivyo.
![](https://matokeochanya.co.tz/wp-content/uploads/2020/08/c6_1-scaled.jpg)
Pombe Magufuli akikagua magari makubwa na madogo 130 yaliyotaifishwa
baada ya kuhusika katika matukio mbalimbali ya uhujumu yaliyohifadhiwa
kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma leo Jumanne Agosti 25, 2020
![](https://matokeochanya.co.tz/wp-content/uploads/2020/08/c7_1-1024x683.jpg)