TUMEPANGA KUNUNUA MELI NANE ZA UVUVI – RAIS DKT. MAGUFULI

Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema kuwa serikali imepanga kununua meli nane za uvuvi ili kuboresha sekta ya uvuvi ili kufikia bahari kuu.

Rais Magufuli amesema hayo wakati akifungua Bunge la 12 mjini Dodoma baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020, amesema kuwa meli hizo zitakazonunuliwa nne zitatumika Zanzibar na nne zitatumiwa Tanzania Bara.

Ad

“Kwa kushirikiana na shirika la IFAD, tumepanga kununua meli nane za uvuvi ambazo zitashiriki katika uvuvi wa bahari kuu katika upande wa Zanzibar na Tanzania Bara, tunakusudia kujenga bandari kubwa ya uvuvi itakayotoa ajira zipatazo 30,000 – Amesema Rais Magufuli

Aidha, amesema kuwa Serikali itakuza shughuli za uvuvi katika maziwa makuu na mito mikubwa, na kuhamasisha wavuvi wadogo kujiunga kwenye vikundi ili kuweze kuwapatia mitaji, ujuzi, vifaa na zana za uvuvi pia, na kupitia upya tozo na kuwapunguzia kero na kuvutia uwekezaji

Ad

Unaweza kuangalia pia

Mitazamo ya Uongozi ya Mhe. Ummy Ally Mwalimu katika Sekta za Afya, Maendeleo ya Jamii, na Haki za Watoto

Ummy Ally Mwalimu ameonyesha mitazamo ya uongozi yenye mwelekeo wa kujali maendeleo na ustawi katika …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *