MAKAMU WA RAIS SAMIA AKUTANA NA MAKAMISHNA WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameipongeza Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora kwa kazi nzuri inayofanywa na Tume hiyo kwa kuweza kutatuwa Changamoto mbalimbali za Wananchi na kuweza kupata Haki zao pale wanapozulumiwa.

Makamu wa Rais amesema hayo leo alipokutana na Ujumbe wa Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora  uliyoongozwa na Mwenyekiti wa Tume Hiyo Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu walipomtembelea kwenye Makazi yake Kilimani Jijini Dodoma.

Ad
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu aliyeongoza Ujumbe wa Makamishna wa Tume wakati Ujumbe huo ulipomtembelea Makamu wa Rais kwenye Makazi yake Kilimaji Jijini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Aidha Makamu wa Rais ameipongeza Tume hiyo kwa kuweza kubadilika na kufanya kazi vizuri pamoja na  kutenda Haki kwa Wananchi na Taasisi zote kwa ujumla.

Nae Mwenyekiti wa Tume ya haki za Binaadamu na Utawala Bora Jaji Msaafu Mathew  Mwaimu ameipongeza Serikali kwa kuweza kuwaletea Wananchi maendeleo Bora na kuitakia kila la heri katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Jaji Mwaimu amesema kuwa Tume yake haipendezewi na vitendo vya baadhi ya Viongozi wa Vyama vya Siasa ambao wamekuwa  wakisema Watu baada ya kunadi Sera za Vyama vyao.

Ad

Unaweza kuangalia pia

Serikali ya Tanzania na Czech Zakubaliana Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili

Serikali za Tanzania na Czech kukuza ushirikiano wa kiuchumi na kuvutia uwekezaji kati yao. Kuondoa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *