Matokeo ChanyA+

Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+.

RAIS MAGUFULI AIPONGEZA MAHAKAMA NA WADAU KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Rais  Dkt. John  Magufuli ameipongeza Mahakama na wadau wake kwa hatua kubwa za kimaendeleo zilizopigwa katika kipindi cha miaka 4 iliyopita na ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha Mahakama inaboreshwa zaidi. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo tarehe 06 Februari, 2020 katika sherehe za kilele cha Wiki ya Elimu na Siku ya …

Soma zaidi »

TRA – WAFANYABIASHARA MSIJIHUSISHE NA BIASHARA ZA MAGENDO

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara na wachuuzi wanaoishi jirani na fukwe za Bahari ya Hindi kutojihusisha na biashara za magengo kwani kufanya hivyo ni kuisababishia nchi kukosa mapato yake stahiki kutokana na wahusika wa biashara hizo kukwepa kulipa kodi. Akizungumza na wafanyabiashara hao katika fukwe za bahari za …

Soma zaidi »

NCHI ZA SADC ZATAKIWA KUTATHMINI UCHUMI WAKE BILA KUTEGEMEA MASHIRIKA YA KIMATAIFA PEKEE

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango amesema kuwa nchi za Afrika hasa zilizopo chini ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) zinatakiwa kujitazama na kushauriana kuhusu mwenendo wao wa uchumi badala ya kuyaachia Mashirika ya Kimataifa pekee. Rai hiyo imetolewa Jijini Dodoma wakati wa …

Soma zaidi »

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA KATIBU MTENDAJI SADC, BALOZI WA EU NA BALOZI WA CHINA

Rais Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 05 Februari, 2020 amekutana na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Mhe. Dkt. Stergomena Tax, Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini Mhe. Manfred Fanti na Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke, Ikulu Jijini Dar es Salaam. …

Soma zaidi »

KATIBU MKUU DKT. ABBASI ASISITIZA MAGEUZI YA KIUTENDAJI KWA MENEJIMENTI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dkt.Hassan Abbasi amewataka viongozi wa menejimenti wa Wizara hiyo kufanya mageuzi kwa kuwa sekta za wizara  hiyo zimebeba ushawishi mkubwa kwa nchi  na dunia. Dkt.Abbasi ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma baada kuwasili katika ofisi ya wizara hiyo iliyopo Mji wa Serikali Mtumba …

Soma zaidi »

BILIONI 8 KUJENGA MAABARA YA KISASA YA UCHUNGUZI MAGONJWA AMBUKIZI HOSPITALI YA KIBONGO’OTO

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatarajia kutumia kiasi cha shilingi Bilioni Nane (8) kwa ajili ya ujenzi wa Maabara kubwa na ya kisasa ya uchunguzi wa magonjwa ambukizi ikiwemo ya Kifua Kikuu katika Hospitali maalum ya Magonjwa ya kuambukiza Kibong’oto, mkoani hapa. Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa …

Soma zaidi »