Taarifa Vyombo vya Habari

WAZIRI LUKUVI AWATAKA WAFUGAJI KUWEKA UZIO ILI KUEPUSHA MIGOGORO NA WAKULIMA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ameagiza wafugaji wote wanaomiliki maeneo yenye hati kuweka uzio katika maeneo yao ili kuepuka mifugo yao kwenda maeneo ya wakulima na kusisitiza kufanyika ufugaji wa kisasa. Lukuvi alitoa agizo hilo wilayani Kilosa mkoani Morogoro wakati akizungumza na uongozi wa wilaya ya Kilosa …

Soma zaidi »

KIKUNDI CHA WAKE WA VIONGOZI CHAKABIDHI MADARASA MANNE NA VYOO KUMI KWA KUTUO CHA WATOTO WENYE MAHITAHJI MAALUM CHA BUHANGIJA

Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa ametoa wito kwa wazazi na walezi watoto wenye mahitaji maalumu  kutowaficha na kuwatelekeza na badala yake wawape nafasi ya kupata elimu kwa sababu ni haki yao ya msingi. Mama Majaliwa ambaye pia ni Mlezi wa Umoja wa Wake wa Viongozi (New Mellenium Women …

Soma zaidi »

JKCI WAFANYA UPASUAJI WA KUTENGANISHA MSHIPA WA DAMU WA KUSAMBAZA DAMU KWENYE MWILI KWA WATOTO

  11/11/2019 Kwa mara ya kwanza madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wamefanya upasuaji wa kutenganisha mshipa wa damu wa kusambaza damu kwenye mwili na kuweka mshipa bandia wa kusambaza damu kwenye mapafu (Truncus Arteriosus). Upasuaji huo uliochukuwa muda wa masaa …

Soma zaidi »

RAIS MAGUFULI AHUTUBIA MKUTANO WA 18 WA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA NORDIC NA AFRIKA

Rais Dkt. John Magufuli amezishukuru nchi za Nordic kwa uhusiano na ushirikiano wake mzuri na nchi za Afrika ikiwemo Tanzania na ametoa wito kwa nchi hizo kujielekeza zaidi katika ushirikiano wa kiuchumi. Mhe. Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 08 Novemba, 2019 alipohutubia Mkutano wa 18 wa Mawaziri wa Mambo …

Soma zaidi »

GESI TULIYONAYO LAZIMA ITUMIKE KUJENGA UCHUMI WA VIWANDA – DKT KALEMANI

Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani amesema mpango wa serikali wa miaka 30 wa matumizi sahihi ya rasilimali za gesi na mafuta, pamoja na mambo mengine, umelenga kuhakikisha gesi inatumika kujenga uchumi wa viwanda. Akizungumza katika ufunguzi wa Jukwaa la Tisa la Uziduaji, Novemba 6, mwaka huu jijini Dodoma, Dkt …

Soma zaidi »

RAIS MAGUFULI: SISI TUNAUWEZO, FURSA NA MAZINGIRA YA KUINGIA KWENYE USHIRIKIANO MADHUBUTI WA KIUCHUMI

Mustakabali wa Taifa letu hauwezi kuwa na maana sana, endapo taifa letu litaendelea kuwa tegemezi kiuchumi. Pamoja na uhusiano mzuri na mafanikio makubwa yaliyopatikana kwenye ushirikiano kati ya nchi za Afrika na Nordic, bado tuna fursa ya kuukuza uhusiano wetu na kuupa msukumo mpya ili kuleta manufaa makubwa zaidi kwa …

Soma zaidi »

HATUTAONGEZA MUDA – DKT KALEMANI

Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani amekataa maombi ya mkandarasi kampuni ya KEC International Ltd kutoka India, anayetekeleza mradi wa kupanua kituo cha kupoza umeme kilichopo Zuzu, mkoani Dodoma, kuongezewa miezi mitatu zaidi ili akamilishe kazi hiyo. Badala yake, Dkt Kalemani amemtaka Mkandarasi huyo kukamilisha kazi husika na kuikabidhi kabla …

Soma zaidi »

TANZANIA YASHIRIKI MAONESHO YA PILI YA KIMATAIFA YA BIDHAA ZA NJE NCHINI CHINA

Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa ameshiriki katika maonesho ya pili ya Kimataifa ya Bidhaa za Nje (CIIE) yanayofanyika nchini China ambayo yamefunguliwa na Rais wa China Xi Jinping ambapo nchi zaidi ya 64 zinashiriki kuonyesha bidhaa mbalimbali. Tanzania inashiriki maonesho hayo kwa kutangaza mazao ya kimakakati pamoja na …

Soma zaidi »