Taarifa ya Habari

BODI YA MIKOPO, YATANGAZA SIFA NA UTARATIBU WA KUOMBA MIKOPO KWA 2019-2020

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza mwongozo wa utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 unaotaja sifa, vigezo na utaratibu wa kuwasilisha maombi ya mikopo ya elimu ya juu na kuwasihi waombaji mikopo watarajiwa kuusoma kwa makini na kuuzingatia. Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru …

Soma zaidi »

WAZIRI BITEKO AKUTANA NA KAMPUNI YA UWEKEZAJI YA NGWENA

Waziri wa Madini Doto Biteko amekutana na Mwekezaji wa Kampuni ya Ngwena Tanzania Ltd “Ngwena” na kufanya nao mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali, kubwa likiwa ni kutoa Ufafanuzi kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Madini inavyotoa fursa na mazingira mazuri ya uwekezaji katika sekta ya madini hapa nchini.  Hatua hiyo inafuatia ombi …

Soma zaidi »

TAASISI ZA FEDHA ZATAKIWA KUCHANGAMKIA VIWANDA VYA USINDIKAJI MAZIWA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo,Profesa Elisante Ole Gabriel amezitaka taasisi za fedha nchini kuchangamkia fursa ya soko la usindikaji wa maziwa ambalo linahitaji uwekezaji wa kimkakati kutokana na sehemu ndogo ya maziwa yanayotoka kwa wafugaji ndiyo yanayosindikwa. Profesa Ole Gabriel ametoa rai hiyo katika kongamano la 10 la Wiki …

Soma zaidi »

CRDB BENKI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUWEZESHA MITAJI KWA WAJASIRIAMALI VIJANA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Majid Nsekela ameipongeza Serikali ya awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mh Rais Dr John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi kubwa inayofanya katika kuleta maendeleo na kuwahudumia Watanzania na hivyo katika kuunga mkono juhudi za serikali Benki ya CRDB ipo tayari kushirikiana na …

Soma zaidi »

MKUTANO WA NISHATI KWA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAANZA ARUSHA

Mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki, umeanza  Juni 3, 2019 jijini Arusha. Akifungua Mkutano huo katika siku ya kwanza ambao unahusisha ngazi ya wataalamu wa sekta husika; Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Fedha na …

Soma zaidi »

TUTAFANYA MAGEUZI KWENYE JUMUIYA ZA HIFADHI ZA WANYAMAPORI – NAIBU WAZIRI KANYASU

Serikali imewahakikishia Wenyeviti wa Muungano wa Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori nchini (WMAs) kuwa itaendelea kufanya mageuzi pamoja na kuwapa ushirikiano kwa kuendeleza dhana halisi ya uhifadhi wa wanyamapori shirikishi katika jamii. Hayo yamebainishwa  jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Constantine Kanyasu wakati akizungumza na wenyeviti …

Soma zaidi »

KITUO CHA TV CHA HAINAN CHA CHINA KUTENGENEZA KIPINDI MAALUM CHA KUTANGAZA BIDHAA ZA TANZANIA

Kituo cha Television cha Hainan nchini China kimeingia makubaliano na Ubalozi wa Tanzania Beijing kutengeneza kipindi maalum cha kutangaza bidhaa za Tanzania, utamaduni, vyakula na utalii katika soko la China ambapo Kipindi hicho kitatengenezwa Mwezi Julai na kurushwa mwezi Novemba 2019 Makubaliano hayo yamefikiwa Beijing katika mkutano wa Balozi wa …

Soma zaidi »