“Leo nimepita eneo nimekuta Bank Kuu.. na wenyewe Benk ya Biashara NBC.. wananiambia, sisi tuko tayari kutoa mikopo kwa wajasiliamali (wa Madini); ili wanunue mitambo, wanunue vifaa vingine vya kusaidia kuchimba.. lakini pia na kuboresha.” – Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.
30/09/2018, Geita
“Benki Kuu wanasema, ni nyie tu (wachimbaji wa madini) mnachelewa kwenda kuomba mikopo.” Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
30/09/2018, Geita
“Na sio lazima uende Benk Kuu.. nilimuuliza swali, we benki Kuu uko Mwanza; Huyu mchimbaji mdogo yuko yuko Nyarugusu anakupataje? Wakaniambia, sio lazima aje Benki Kuu. Kila benki NMB, CRDB, NBC na benki nyingine yoyote ukienda..ukienda mikopo kwa ajili ya madini.. Benk Kuu itakudhamini..” – Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu
30/09/2018, Geita.
“Fomu utakayopewa kujaza (kuombea mkopo katika benki husika) itakuonyesha kipengele cha kwenda Benki Kuu kwenda kukudhamini; Kwahiyo mnakopesheka! Tunachozungumza ni cha uhakika.. tumezungumza na mabenki sasa yajiimarishe kukopesha wajasiliamali wadogo wadogo, wachimbaji wadogo wadogo kwenye sekta ya Madini na wafanyabiashara wengine. Msihofu; Nenda mkakope.. ndio njia pekee ya kupata mtaji wa Uhakika.” – Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa
30/09/2018, Geita.