Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo
Jumapili Agosti 23,. 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dodoma
Mhashamu Beatus Kinyaiya aliposhiririki Misa Takatifu ya Dominika ya
21 ya Mwaka “A” na kuzindua Kanisa, Nyumba ya Mapadres na Grotto ya
Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo Jumapili Agosti
23,. 2020
Rais Dkt. John Magufuli amezindua Kanisa, nyumba ya Mapadre na Groto katika Parokia ya Bikira Maria Imakulata, Ikulu Chamwino iliyopo Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma.
Katika uzinduzi huo, Rais Magufuli ameambatana na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma, Mhashamu Beatus Kinyaiya ambaye amelibariki Kanisa, Groto na nyumba ya Mapadre na baadaye kuongoza Misa Takatifu ya Dominika ya 21 ya Mwaka “A” ndani ya Kanisa hilo.
Ad
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akishukuru baada ya kukabidhi michango kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la
Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya aliposhiririki iliyotokana na harambee
kuchangia ujenzi wa Msikiti wa Chamwino wakati wa Misa Takatifu ya
Dominika ya 21 ya Mwaka “A” ambapo pia alizindua Kanisa, Nyumba ya
Mapadres na Grotto ya Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino
leo Jumapili Agosti 23,. 2020
Ujenzi wa Kanisa la Bikira Maria Imakulata, Ikulu Chamwino, Groto na ukarabati wa nyumba ya Mapadre wa Kanisa hilo ulianza tarehe 08 Juni, 2020 siku moja baada ya Rais Magufuli kuhudhuria Ibada ya Fumbo la Utatu Mtakatifu na kisha kuendesha harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa hilo ambapo pamoja nae, Waumini wa Kanisa hilo na Madhehebu mbalimbali ya Kikristo na Kiislamu wamejitokeza kuchangia na kufanikiwa kukamilisha ujenzi huo.
Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) Padre Dkt. Charles Kitima amemshukuru Rais Magufuli kwa upendo na uamuzi wake wa kufanya ujenzi mkubwa wa Kanisa, Groto na kukarabati nyumba ya Mapadre wa Parokia hiyo ambayo kwa kuwa kwake Ikulu Chamwino ina historia ya kuwahudumia Marais wa Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akiendesha harambee kuchangia ujenzi wa Msikiti wa Chamwino
wakati wa Misa Takatifu ya Dominika ya 21 ya Mwaka “A” ambapo pia
alizindua Kanisa, Nyumba ya Mapadres na Grotto ya Parokia ya Bikira
Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo Jumapili Agosti 23,. 2020
Baba Askofu Mkuu Kinyaiya amemshukuru Rais Magufuli kwa kuongoza kazi kubwa iliyofanyika kuiboresha Parokia ya Bikira Maria Imakulata, Ikulu Chamwino na amemuelezea kuwa ni kiongozi mwenye uthubutu na anayejali watu anaowaongoza.
Katika Ibada hiyo, Baba Askofu Mkuu Kinyaiya amembariki na kumuombea Rais Magufuli ili aendelee kuliongoza Taifa vizuri na hasa wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu, na pia amewataka Watanzania wote kushiriki uchaguzi mkuu huku wakidumisha amani na mshikamano, na kuhakikisha wanachagua viongozi wacha Mungu, wanaotafuta uongozi kwa njia za amani, wanaojiamini na wasiotoa rushwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akipokea michango kutoka kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dodoma
Mhashamu Beatus Kinyaiya kwa ajili ya ujenzi wa Msikiti wa Chamwino
baada ya kuitisha Harambee aliposhiririki Misa Takatifu ya Dominika
ya 21 ya Mwaka “A” ambapo pia alizindua Kanisa, Nyumba ya Mapadres na
Grotto ya Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo
Jumapili Agosti 23,. 2020
Katika salamu zake, Rais Magufuli amemshukuru Baba Askofu Mkuu Kinyaiya kwa kuongoza Misa Takatifu na kulibariki Kanisa, Groto na Nyumba ya Mapadre, na pia amewashukuru wote waliojitokeza kuchangia ujenzi na ukarabati huo ambao umefanyika kwa mafanikio makubwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akikabidhi michango kwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dodoma Mhashamu
Beatus Kinyaiya aliposhiririki iliyotokana na harambee kuchangia
ujenzi wa Msikiti wa Chamwino wakati wa Misa Takatifu ya Dominika ya
21 ya Mwaka “A” ambapo pia alizindua Kanisa, Nyumba ya Mapadres na
Grotto ya Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo
Jumapili Agosti 23,. 2020
Rais Magufuli ameelezea kufurahishwa na umoja wa Watanzania ulioneshwa katika ujenzi huo ambapo waliojenga na waliochangia fedha wametoka katika Madhehebu mbalimbali ya Dini.
Akiwa anatoa salamu hizo, Rais Magufuli ameamua kuendesha harambee nyingine ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Msikiti wa Waislamu wa Chamwino ambapo amefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi Milioni 48, mifuko 48 ya saruji na tripu 5 za mchanga kutoka kwa Waumini wa Parokia ya Bikira Maria Imakulata na Waumini wa Madhehebu mengine mbalimbali waliojitokeza papo hapo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akikagua msikiti wa Chamwino na maemneo yake baada ya kuendesha
harambee ya kuchangia ujenzi wake wakati wa Misa Takatifu ya Dominika
ya 21 ya Mwaka “A” wakati wa uzinduzi wa Kanisa, Nyumba ya Mapadres na
Grotto ya Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo
Jumapili Agosti 23,. 2020Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
katika picha ya pamoja na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dodoma Mhashamu
Beatus Kinyaiya, Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania )TEC) Padri
Dkt. Charles Kitima na Paroko wa Kanisa hilo Paul Mapalala baada ya
kushiriki Misa Takatifu ya Dominika ya 21 ya Mwaka “A” ambapo pia
alizindua Kanisa, Nyumba ya Mapadres na Grotto ya Parokia ya Bikira
Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo Jumapili Agosti 23,. 2020Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akishiriki na waumini wengine katika Misa Takatifu ya Dominika ya 21
ya Mwaka “A” ambapo pia alizindua Kanisa, Nyumba ya Mapadres na Grotto
ya Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo Jumapili
Agosti 23,. 2020