RAIS MAGUFULI ATANGAZA SIKU 7 ZA MAOMBOLEZO YA KITAIFA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza siku 7 za maombolezo ya Kitaifa kuanzia leo Ijumaa tarehe 24 Julai, 2020 kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa kilichotokea Jijini Dar es Salaam.

Katika kipindi chote cha maombolezo bendera zote zitapepea nusu mlingoti.

Ad

Rais Magufuli amewaomba Watanzania wote kuendelea kuwa watulivu, wastahimilivu na wamoja katika kipindi hiki kigumu cha majonzi ya kuondokewa na mpendwa wao, Rais Mstaafu Mkapa.

Taarifa zingine kuhusiana na msiba huu mkubwa kwa Taifa zitatolewa baadaye.

Ad

Unaweza kuangalia pia

Mafanikio Na Umuhimu Wa Muungano Wa Tanzania: Sababu Za Kuunganisha Tanganyika Na Zanzibar

Kuunganisha Tanganyika na Zanzibar kulilenga kujenga umoja wa kitaifa na kuvunja mipaka ya kikanda na …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *