Meja Jenerali Martin Busungu, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini akikagua askari wa Kikosi cha JKT Mafinga mara baada ya kuwasili ili kukagua na kujionea shughuli mbalimbali za uzalishaji mali zinazofanywa na kikosi hicho.

MKUU WA JKT AFANYA ZIARA YA KIKAZI KIKOSI CHA MAFINGA JKT

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Tanzania (JKT) Meja Jenerali Martin Busungu Ijumaa tarehe 05/10/2018 ametembelea kikosi cha JKT Mafinga na kukagua shughuli mbalimbali za uzalishaji mali zinazofanywa na kikosini hapo.

JKT-MAFINGA-7.png
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Martin Busungu akisalimiana na maafisa wa Jeshi wa kikosi cha JKT Mafinga katika ziara yake ya kujitambulisha na kukagua shughuli mbalimbali za uzalishaji mali pamoja na mafunzo ya vikosi vya jeshi hilo.

 

Ziara hiyo ya Mkuu wa jeshi la Kujenga Taifa ni muendelezo wa ziara zake za kujitambulisha na kujionea shughuli za uzalishaji mali kwenye vikosi vya JKT nchini.

Ad
JKT-MAFINGA-5.png
Pichani, Meja Jenerali Busungu akisalimiana na askari wa JKT katika kikoso cha Mafinga

 

MKUU WA JKT MEJA JENERALI BUSUNGU
Meja Jenerali Martin Busungu, Mkuu wa JKT akipata maelezo ya kitaalam kuhusu shughuli za ufugaji unaofanyika katika Kikosi cha JKT Mafinga – Mufindi mkoani Iringa.
MEJA JENERALI MARTIN BUSUNGU. MKUU WA JESHI LA KUJENGA TAIFA
Meja Jenerali Busungu akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye Kikosi cha JKT Mafinga kwa ziara maalum ya kujitambulisha na kujionea shughuli za uzalishaji mali zinazofanywa na kikosi hicho cha jeshi analoliongoza.

 

JKT-MAFINGA-1.png
Meja Jenerali Busungu akisikiliza maelezo kuhusu shughuli za kilimo alipoingia katika ghala la kuhifadhia chakula baada ya mavuno kwenya mashamba ya kikosi cha JKT Mafinga.

 

MEJA JENERALI BUSUNGU KATIKA PICHA YA PAMOJA NA UONGOZI WA JKT MAFINGA
Mkuu wa jeshi la Kujenga Taifa nchini, Meja Jenerali Martin Busungu akipiga picha ya kumbukumbu na uongozi wa kikosi cha JKT Mafinga
JKT-MAFINGA-11.png
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Busungu akiongea na askari wa kikosi cha JKT Mafinga.
Ad

Unaweza kuangalia pia

WATUMISHI FANYENI KAZI KWA UADILIFU, UTIIFU NA WELEDI – SHIGELA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela amewataka watumishi wa Umma kufanya kazi kwa kuzingatia …

2 Maoni

  1. Kazi nzuri sana inayofanywa na JKT kwa ujumla. Tunatakiwa tuwatie moyo zaidi lakini tuongeze fursa za kutangaza yale wanayofanya ili na wananchi wajue kazi nzuri na umuhimu wake kwa jamii kabla ya hatua kubwa.

    Tukikaa kimya bila kutangaza mafanikio yao ni vigumu jamii kujua kazi kubwa ya JKT hususan katika enzi hizi za mabadiliko makubwa kuelekea Tanzania ya viwanda

  2. Mimi Agonza lvan joel ni kijana wa mtanzania mwenye umri wa miaka 25 nina diploma ya computer science nilikuwa naomba hatua za kujiunga na tarehe ya nafasi za kujiunga na JKT maana nina nia ya kulitumikia taifa langu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.