Yakubali kampuni yake ya Acacia ilifanya makosa katika kuendesha shughuli zake nchini.
Ni baada ya kubainika kwa wizi wa madini katika makinikia na serikali kuzuia makontena yote bandarini, Mkuu wa Barrick alijitokeza na kuomba suluhu wayamalize.
Baada ya siku chache, timu ya viongozi waandamizi na wanasheria wa Barrick, walifika nchini tayari kwa mazungumzo na serikali.
Miezi michache baadae, makubaliano ya awali yalifikiwa na kusainiwa mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Na sasa nchi yetu, iko tayari kupokea fidia na malimbikizo ya kodi iliyokwepwa.
Mhe. Prof. Paramagamba Kabuni, Waziri wa Sheria na Katiba alisema, “Watanzania tuna kila sababu ya kusema tumepiga hatua kuliko wale waliotutangulia katika jambo hili (Majadiliano kati ya Seriakli ya Tanzania na kampuni ya Barrick Gold Corporation) Na kwa hali hiyo kabisa nirudie tena, nimshukuru tena Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.. kwa lugha ya mtaani kwa ‘kuliamsha hili dude’. Baada ya hili dude kuamka, ambalo lilianzia kwenye makinikia.., na watu wengi walidhani issue yetu ni makinikia.. sisi tulivyokwenda kwenye majadiliamno tulikuwa na mambo makuu matano.. nje ya makinikia. Lengo letu lilikuwa kuyatumia mazungumzo haya kama alivyotuelekeza mwenyewe Mhe. Rais.. kufungua mwelekeo mpya wa usimamizi wa maliasili ya nchi yetu ikiwemo madini. – Profesa Paramagamba Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria
Tazama video
Ad
fuatilia hotuba ya Rais Magufuli akipokea ripoti ya mchanga wa madini
Ni jambo la kujivunia nawapongeza viongozi wetu wote waliosimamia swala hili kwa uaminifu na umakini wa hali ya juu Mhe. Rais John Pombe Magufuli nakuombea kwa mungu akulinde na ma waziri na wengine wote na mimi binafsi lilikua likiniumiza roho sana
Nampongeza Rais wa Tanzania J.P.Magufuli na kuwapongeza wote walosimamia jambo hili kwa msimamo mmoja bila kurudi nyuma na hatimaye kuleta natija nzuri ya mafanikio.Hongereni saana.Tunamatumaini makubwa sana kwa umoja wenu huu Nchi yetu itajikomboa na mabepari wanyonyaji wasiokuwa na huruma na mali ya Wananchi.Mungu Ibariki Tanzania, wabariki watu wake wote, waongoze wawe wamoja daima, waijenge Tanzania kwa manufaa ya wote.Ameen
Ni jambo la kujivunia nawapongeza viongozi wetu wote waliosimamia swala hili kwa uaminifu na umakini wa hali ya juu Mhe. Rais John Pombe Magufuli nakuombea kwa mungu akulinde na ma waziri na wengine wote na mimi binafsi lilikua likiniumiza roho sana
Nampongeza Rais wa Tanzania J.P.Magufuli na kuwapongeza wote walosimamia jambo hili kwa msimamo mmoja bila kurudi nyuma na hatimaye kuleta natija nzuri ya mafanikio.Hongereni saana.Tunamatumaini makubwa sana kwa umoja wenu huu Nchi yetu itajikomboa na mabepari wanyonyaji wasiokuwa na huruma na mali ya Wananchi.Mungu Ibariki Tanzania, wabariki watu wake wote, waongoze wawe wamoja daima, waijenge Tanzania kwa manufaa ya wote.Ameen