FUAD: TUKO TAYARI KUPOKEA NAKUSAFIRISHA MIZIGO NA VIFAA VYA UJENZI MRADI WA UMEME RUFUJI.

  • Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) limekamilisha ujenzi na ukarabati wa Stesheni ya Treni Fuga uliohusisha Stendi kubwa ya kupokea mizigo na vifaa vya ujenzi wa bwawa la kufua Umeme Mto Rufuji.
  • Akizungumza katika ziara ya kutembelea ujenzi wa huo, Meneja wa Shirika hilo nchini Tanzania, Fuad Abdallah amasema kuwa Serikali ya jamuhuri ya Tanzania imewapa dhamana kubwa ya kutekeleza ujenzi wa stendi hiyo ya kutunzia vifaa vya ujenzi kwa hiyo ni historia kubwa kwa shirika hilo kushiriki katika mageuzi ya kwenda uchumi wa kati wenye viwanda.
  •  Fuad Abdallah amesema kuwa reli ya TAZARA ipo bega kwa bega katika kutekelezaji wa agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kushiriki ujenzi wa mradi mkubwa wa kuzalisha umeme na kazi ambayo ilitakiwa kutekelezwa tayari imemalizika kwa sasa stesheni hiyo iko tayari kupokea mizigo kwa matumizi ya ujenzi wa mradi mkubwa wa kufua umeme mto Rufiji.
  • “TAZARA inajukumu kubwa sana la kuhakikisha mizigo yote mizito inayotakiwa kujenga mradi huu mkubwa wa Serikali, inafika kwa usalama na kwa wakati katika stesheni yetu lakini pia mahali ambapo mradi unajengwa, kwa matumizi ya reli inamaana kuwa kuna mizigo mingine haiwezi kupita barabarani hivyo TAZARA ni jukumu letu kuhakikisha atucheleweshi mradi huu kwa kufikisha malighafi za ujenzi kwa wakati” alisema Fuad Abdallah.
  • Fuad alisema kuwa Serikali imeimarisha miundombinu ya umeme, maji, vyumba vya kulala na kituo cha kufikia mizigo,kuhifadhi na kusafiriha mizigo, na itajikita zaifdi katika kuboresha miundombinu ya Reli hiyo ambayo inategemewa zaidi katika usafirishaji wa mizigo ya ujenzi wa mradi wa kufua umeme Mto Rufiji.
  • Kwa upande wake msimamizi wa mradi wa ukarabati wa fuga stesheni, Gideon Mubepi, alisema kuwa kituo hicho cha fuga Stesheni pamoja na Reli  ya kushushia mizigo kimekamilika kwa asilimia mia moja, na kwa wakati mbali na changamoto zilizokuwepo wakati wa ujenzi.
  • Naye Kamanda wa Polisi TAZARA, ACP Debora Magiligimba alisema kuwa Jeshi la Polisi TAZARA wamejipanga kimamilifu kuhakikisha mizigo inayotakiwa kufika katika mradi huo mkubwa itakuwa salama na kuwezesha mradi huo wa kufua umeme kukamilika kwa wakati.
  • “Jeshi la Polisi TAZARA, tumejipanga kuhakikisha ulinzi wa vifaa vyote vinavyoshushwa hapa, na ata pale vinavyochukuliwa kwa ajili ya kupelekwa kwenye mradi husika” ACP Debora Magiligimba
  • Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Dkt. Tito Mwinuka alisema kuwa  utekelzaji huo wa ujenzi wa bwawa la  kufua umeme utarahisika kwa sababu ya kituo hicho cha  kupokea na kusafirisha,  mizigo na vifaa vya ujenzi, kimefanyiwa ukarabati mkubwa na sasa kipo tayari,hasa uwepo wa stendi ya kuifadhi malighafi za ujenzi katika stesheni ya Fuga.
  • “TAZARA wamefanya kazi nzuri sana, wameandaa kituo hiki cha Fuga na  wamekijenga vizuri sana na tayari kinauwezo wa kupakua,kuhifadhi  na kuisafirisha malighafi za ujenzi kwenda kwenye mradi huu mkubwa wa kufua  umeme katika bonde la Mto Rufiji na sasa tuna uhakika kabisa hakuna mzigo utakao shindwa kufika eneo husika sababu miundombinu yote ipo salama” Dkt. Tito Mwinuka.
Ad

Unaweza kuangalia pia

TPDC YAOKOA TRILIONI 12.7 KUAGIZA MAFUTA NJE YA NCHI

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika kipindi cha miaka minne ya Uongozi wa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *