SOKO LA DHAHABU MKOANI GEITA LACHANGIA MAPATO YA SERIKALI KUPITIA MRABAHA NA ADA YA UKAGUZI KWA JUMLA YA BILIONI 36.57

Na Nuru Mwasampeta, WM

WAZIRI wa Madini, Doto Biteko amewataka Watanzania kuutazama mchango wa sekta ya madini kwa namna unavyosaidia kuinua sekta nyingine za uchumi, kwani tayari kwa upande wa kuongezeka kwa ukusanyaji wa maduhuli sekta hiyo imeonesha mafanikio makubwa.

Ad

“Niliwaambia wenzangu wizarani, lazima tuhame sasa kwenye mfumo wa kufurahia kuona mapato yameongezeka kutokana na ukusanyaji wa maduhuli twende kwenye mfumo wa kujiuliza je? Sekta ya madini imechangiaje ukuaji wa sekta nyingine?.

Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel (kulia) na wajumbe walioambatana nao wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Madini mkoani humo. (Picha na Wizara ya Madini).

“Anayelima mchele awe na uhakika wa wanunuzi kwa sababu wachimbaji wapo, anayefuga ng’ombe awe na uhakika wa soko kwa sababu wanunuzi wapo, anayelima nyanya na shughuli nyingine hivyo hivyo, na huo ndio tunaita ufungamanishaji wa uchumi wa madini na sekta nyingine;

Waziri Biteko aliyabainisha hayo hivi karibuni mkoani Geita alipofanya ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo inayofanywa kwa fedha za huduma za jamii (CSR) zinazotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) ambapo alikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo jipya unaoendelea katika soko kuu la dhahabu Geita pamoja na soko la Katundu litakalohusisha biashara za kawaida lililojengwa katika Halmashauri ya Mji wa Geita.

Pamoja na kukagua miradi ya maendeleo inayowezeshwa na GGML, Waziri Biteko alizungumza na wafanyabiashara wa madini mkoani humo na kueleza kuwa kutokana na changamoto ya Covid-19, wizara imetoa kipindi cha miezi mitatu kwa wafanyabiashara wa madini kununua madini mahali popote nchini na kuwataka kuzingatia uwepo wa vibali vyote muhimu vinavyoonesha mahali madini hayo yamenunuliwa na yanakopelekwa mara baada ya kuyanunua.

Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa tatu kutoka kulia) na ujumbe alioambatana nao ikiwa ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel (kulia kwake) wakikagua ujenzi wa kiwanda cha kuchakata dhahabu kinachojengwa na mwekezaji binafsi mkoani humo. (Picha na Wizara ya Madini).

Akitoa taarifa ya sekta,  Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel amesema mwenendo wa biashara ya madini ya dhahabu katika mkoa wake tangu soko la dhahbu kufunguliwa mwezi Machi 2019 hadi Mei 2020 kipindi cha miezi 14 jumla ya kilo 5,320.99 zenye thamani shilingi Bilioni 522.44 zimeuzwa na kuchangia mapato ya serikali kupitia  mrabaha na ada ya ukaguzi kwa jumla ya shilingi bilioni 36.57.

Amesema, ongezeko hilo linaonesha namna sekta ya madini ilivyokuwa na mafanikio makubwa sana kutokana na usimamizi makini na uongozi bora wa wizara, lakini pia utii na utekelezaji wa ushauri na maelekezo yanayotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Aliongeza kuwa, fedha inayopatikana kutokana na makusanyo kwenye sekta ya madini ndiyo inayokwenda kulipa elimu bure, kujenga vituo vya afya, inatumika katika kujenga hospitali za wilaya na mambo mengine mengi yanayotekelezwa na serikali yetu.

Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza na wafanyabiashara wa madini wa Mkoa wa Geita hivi karibuni alipofanya ziara ili kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi ya maendeleo inayofanywa kwa fedha za huduma za jamii (CSR) zinazotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML) uliopo mkoani Geita. (Picha na Wizara ya Madini).

Amebainisha kuwa, mkoani Geita kuna ongezeko kubwa la viwanda vya kuchenjua dhahabu  (Illusion Plant) kutoka viwanda 20 vilivyokuwepo awali na kufikia viwanda 39 na kubainisha kuwa hayo ni mageuzi makubwa katika sekta ya madini kwa kuwezesha uwepo wa viwanda vidogovidogo mkoani humo.

Ameendelea kusema, kwa mwaka 2018  halmashauri zilizoko katika Mkoa wa Geita zilinufaika kutokana na utekelezaji wa takwa la kisheria la utekelezaji wa mpango wa kuchangia huduma za kijamii ambapo Mgodi wa Geita (GGML) uliotoa kiasi cha shilingi bilioni 9.2 kama mchango wa mgodi kwenye masuala ya kijamii na kupelekea maendeleo ya mkoa huo kwenda kwa kasi.

 Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Geita, Mjiolojia Daniel Mapunda amesema, Mkoa wa Geita una leseni kubwa za utafiti wa madini 283, leseni za uchimbaji mkubwa wa madini 2, leseni 17 za uchimbaji wa kati, leseni 1487 za uchimbaji mdogo wa madini na leseni 384 za uchenjuaji wa madini (illusion plant na vat-reaching plant).

Kwa upande wa leseni za biashara ya madini, Mapunda amesema kuna jumla ya leseni kubwa za biashara ya madini 33 kwenye soko kuu la dhahabu Geita na leseni ndogo za biashara ya madini 69 zilizopo katika vituo vidogovidogo vya ununuzi wa madini zilizotolewa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020.

Akizungumzia mwenendo wa ukusanyaji wa maduhuli ya serikali, Mapunda ameeleza kuwa lengo la makusanyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020 lilikuwa ni kukusanya shilingi bilioni 156.34 ambapo kufikia Juni 2, 2020 kiasi cha shilingi bilioni 191.52 sawa na asilimia 122.5 ya lengo la makusanyo kimekusanywa.

Amesema, makusanyo hayo ni ongezeko la kiasi cha shilingi bilioni 62.54 ukilinganisha na kiasi kilichokusanywa kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Amebainisha kuwa, kati ya hizo jumla ya shilingi bilioni 34.2 zimetokana na shughuli za uchimbaji mdogo wa madini sawa na ongezeko la asilimia 310 ya mapato yaliyopatikana kutokana na uchimbaji mdogo kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo kiasi kilichokusanywa ni shilingi bilioni 11 pekee.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Makamu wa Rais anayeshughulikia Miradi Endelevu (GGML), Simon Shayo, amesema, kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 9 kilitolewa kwa mwaka 2018 ili kuzinufaisha jamii zinazozunguka mgodi huo na kuongeza kuwa mgodi unafurahi kuona wananchi wa kawaida wakiboresha maisha yao kutokana na mgodi kuwepo katika jamii yao.

Katika ziara hiyo, Waziri wa Madini alikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo jipya litakalohusisha wafanyabiashara wengine wa dhahabu katika soko la dhahabu Geita, ujenzi wa soko la Katundu, kukagua kituo cha uwekezaji Bombambili, pia alikagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata madini kinachojengwa na mwekezaji binafsi mkoani humo.

Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS SAMIA ATEMBELEA RUKWA.. AANGAZIA AFYA, ELIMU, KILIMO NA MIUNDOMBINU KWA MIRADI YA MAENDELEO.

Katika ziara ya Rais Samia siku ya leo iliangazia kwenye sekta ya Afya, Elimu, Kilimo …

72 Maoni

  1. Selena Gomez https://calm-down.selenagomez-br.net the story from child star to global musical influence, summarized in hit “Calm Down”, with Rema.

  2. Kobe Bryant https://los-angeles-lakers.kobebryant-br.net one of the greatest basketball players of all the times, left an indelible mark on the history of sport.

  3. Ayrton Senna https://mclaren.ayrtonsenna-br.com is one of the greatest drivers in the history of Formula 1.

  4. Добрый день!
    Мы изготавливаем дипломы психологов, юристов, экономистов и прочих профессий по доступным ценам. Цена будет зависеть от конкретной специальности, года выпуска и образовательного учреждения.
    Где купить диплом специалиста?
    Приобрести диплом о высшем образовании
    landik-diploms-srednee.ru/kupit-diplom-saratov  
    Успешной учебы!

  5. Victor Osimhen https://napoli.victorosimhen-ar.com born on December 29, 1998 in Lagos, Nigeria, has grown from an initially humble player to one of the brightest strikers in modern football.

  6. The story of Leo Messi https://inter-miami.lionelmessi.ae‘s transfer to Inter Miami began long before the official announcement. Rumors about Messi’s possible departure from Barcelona appeared in 2020

  7. Добрый день!
    Где приобрести диплом по необходимой специальности?
    Мы готовы предложить документы институтов, которые расположены на территории всей РФ. Вы можете заказать качественный диплом от любого высшего учебного заведения, за любой год, включая сюда документы старого образца СССР. Дипломы выпускаются на “правильной” бумаге высшего качества. Это дает возможность делать государственные дипломы, не отличимые от оригинала. Они заверяются всеми необходимыми печатями и штампами.
    Мы можем предложить дипломы психологов, юристов, экономистов и других профессий по приятным ценам.
    ast-diploms24.ru/otzyvy
    Рады помочь!

  8. Привет, друзья!
    Где заказать диплом по необходимой специальности?
    mymink.5bb.ru/viewtopic.php?id=8918#p455039
    Удачи!

  9. Добрый день!
    Узнайте стоимость диплома высшего и среднего образования и процесс получения
    komfort.rusff.me/viewtopic.php?id=13950#p41118
    Поможем вам всегда!.

  10. Сайт https://ps-likers.ru предлагает уроки по фотошоп для начинающих. На страницах сайта можно найти пошаговые руководства по анимации, созданию графики для сайтов, дизайну, работе с текстом и фотографиями, а также различные эффекты.

  11. Привет, друзья!
    Как получить диплом о среднем образовании в Москве и других городах
    ya3bbru.bbok.ru/viewtopic.php?id=4043#p7096
    Будем рады вам помочь!.

  12. Luis Diaz https://liverpool.luis-diaz-ar.com is a young Colombian striker who has enjoyed rapid growth since joining the ” Liverpool” in January 2022.

  13. Muhammad Al Owais https://al-hilal.mohammed-alowais-ar.com is one of the most prominent names in modern Saudi football. His path to success in Al Hilal team became an example for many young athletes.

  14. Brazilian footballer Ricardo Escarson https://orlando-city.kaka-ar.com dos Santos Leite, better known as Kaka, is one of the most famous and successful players in football history.

  15. Monica Bellucci https://dracula.monica-bellucci-ar.com one of the most famous Italian actresses of our time, has a distinguished artistic career spanning many decades. Her talent, charisma, and stunning beauty made her an icon of world cinema.

  16. Привет, друзья!
    Купить документ института вы сможете у нас.
    ast-diplomas.com/kupit-diplom-nizhnij-novgorod

  17. Travis Scott https://astroworld.travis-scott-ar.com is one of the brightest stars in the modern hip-hop industry.

  18. Chelsea https://england.chelsea-ar.com is one of the most successful English football clubs of our time.

  19. Добрый день!
    Как получить диплом техникума с упрощенным обучением в Москве официально
    animesocial.su/blogs/2461/Купите-Диплом-для-Вашего-Успеха

  20. Mike Tyson https://american-boxer.mike-tyson-ar.com one of the most famous and influential boxers in history, was born on June 30, 1966 in Brooklyn, New York.

  21. Привет!
    Купить документ института вы можете у нас в столице.
    diplomyx24.ru/kupit-diplom-moskva
    Успехов в учебе!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *