IMF YAAHIDI KUIPATIA TANZANIA FEDHA ITAKAYOIHITAJI

Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi  

Shirika la Fedha Duniani (IMF) limeahidi kuipatia Tanzania fedha itakayoihitaji ili iweze kuendelea kukabiliana na athari zitokanazo na janga la Covid 19 kwa ajili ya kuimarisha uchumi wake.

Mkurugenzi Mkazi wa IMF nchini Tanzania Bw. Jens Reinke ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamamba John Kabudi leo katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Ad
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi akiongea na Balozi wa Vietnam  nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh ambaye amemaliza muda wake wa utumishi nchini Tanzania

Pia Bw. Reinke ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua madhubuti inazozichukua  katika kukabiliana na janga la Covid 19 ili kuepusha madhara ya kiuchumi na kijamii.

Mazungumzo hayo pia yamelenga miradi ya maendeleo, msamaha wa madeni kwa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania, ushirikiano baina ya IFM na Tanzania, biasara na utalii.   

Mkurugenzi Mkazi wa IMF nchini Tanzania Bw. Jens Reinke akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi leo katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam

Kwa upande wake, Prof. Kabudi ameishukuru (IMF) kwa msamaha wa madeni ambao umetolewa kwa Tanzania na nchi nyingine, fedha zitakazoziwezesha nchi hizo kuendelea kukabiliana na Covid 19.

“Tumeongelea mambo mbalimbali yanayohusu ushirikiano hasa katika kuimarisha uchumi wetu baada ya janga la covid 19, usirikiano kati ya Tanzania na IMF unafahamika na tumekubaliana baadhi ya mambo ambayo tutayafanyia kazi kwa kina ili tuweze kuimarisha uchumi wetu baada ya corona hasa katika sekta ya utalii, biashara na miundombinu,” amesema Prof. Kabudi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa IMF nchini Tanzania Bw. Jens Reinke

Katika hatua nyingine, Waziri Kabudi amekutana na kumuaga Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Kim Doanh ambaye amemaliza muda wake wa utumishi na amemtakia maisha mema na kumsihi kuendelea kuwa balozi mwema kwa Tanzania nchini Vietnam na duniani kwa ujumla.

“Kwa niaba ya Serikali napenda kukuhakikishia kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Vietnam katika nyanja mbalimbali za kimataifa ikiwemo kuiunga mkono Vietnum katika kugombea nafasi mbalimbali katika Masirika ya KImataifa,” Amesema Prof. Kabudi

Nae Balozi Doanh ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano ambao imekuwa ikimpatia alipokuwa akitekeleza majukumu yake nchini wakati wote na kuahidi kuwa ushirikiano kati ya nchi hizo mbili utaendelea kuimarishwa.

Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS SAMIA ATEMBELEA RUKWA.. AANGAZIA AFYA, ELIMU, KILIMO NA MIUNDOMBINU KWA MIRADI YA MAENDELEO.

Katika ziara ya Rais Samia siku ya leo iliangazia kwenye sekta ya Afya, Elimu, Kilimo …

111 Maoni

  1. In 2018, the basketball world witnessed one of the most remarkable transformations in NBA history. LeBron James https://los-angeles-lakers.lebronjames-ar.com one of the greatest players of our time, decided to leave his hometown Cleveland Cavaliers and join the Los Angeles Lakers.

  2. Luis Diaz https://liverpool.luis-diaz-ar.com is a young Colombian striker who has enjoyed rapid growth since joining the ” Liverpool” in January 2022.

  3. Kevin De Bruyne https://manchester-city.kevin-de-bruyne-ar.com is a name every football fan knows today.

  4. Казахский национальный технический университет https://satbayev.university им. К.Сатпаева

  5. Kylie Jenner https://kylie-cosmetics.kylie-jenner-ar.com is an American model, media personality, and businesswoman, born on August 10, 1997 in Los Angeles, California.

  6. Bella Hadid https://img-models.bella-hadid-ar.com is an American model who has emerged in recent years as one of the most influential figures in the world of fashion.

  7. Edson Arantes https://santos.pele-ar.com do Nascimento, known as Pele, was born on October 23, 1940 in Tres Coracoes, Minas Gerais, Brazil.

  8. Priyanka Chopra https://baywatch.priyankachopra-ar.com is an Indian actress, singer, film producer and model who has achieved global success.

  9. Muhammad Ali https://american-boxer.muhammad-ali-ar.com is perhaps one of the most famous and greatest athletes in the history of boxing.

  10. Manny Pacquiao https://filipino-boxer.manny-pacquiao-ar.com is one of the most prominent boxers in the history of the sport.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *