UJENZI WA OFISI ZA PAPU KUGHARIMU SHILINGI BILIONI 33.7

Serikali yaridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo la ghorofa 17 za ofisi ya Makao Makuu ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU) unaoendelea kufanyika mkoani Arusha

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula ambapo jana alitembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa ofisi hizo mkoani humo akiwa ameambatana na viongozi wengine wa Serikali na PAPU akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo; Katibu Mkuu wa Wizara ya Katibu na Sheria, Prof. Sifuni Mchome; Naibu Katibu Mkuu wa Sekta ya Mawasiliano, Dkt. Jim Yonazi; Katibu Mkuu Msaidizi wa PAPU, Kolawole Aduloju; na watendaji wengine wa Halmashauri ya Jiji la Arusha; na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania

Ad

Dkt. Chaula amesema kuwa ujenzi wa ofisi za PAPU utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 33.7 na ni mradi wa kimkakati na wa kibiashara nchini hususan kwa biashara posta nchini ambapo inategemewa kukua kupitia mradi huu ambapo lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendelea kukua zaidi kiuchumi na posta ni sehemu ya mkakati na ndio maana tunapitia mradi huu kila wakati ili kuhakikisha kuwa mradi huu unatekelezwa vizuri

Na Prisca Ulomi, WUUM, Arusha

Ameongeza kuwa Serikali imejenga Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano na inahimiza matumizi TEHAMA, Shirika la Posta Tanzania (TPC) linatumia magari kutoa huduma zake kwa wateja ambapo moja ya jukumu lake ni kufanya biashara hivyo TPC anatumia biashara mtandao kwa kuingia makubaliano na muuzaji na mnunuzi wa bidhaa kutoka nchi yeyote na zinakuja Tanzania na TPC anakuwa msafirishaji mkuu, hii ni fursa na ni jukumu langu kuhakikisha mawasiliano haya yanaendelea kukua hususani kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano

Naye msimamizi wa ujenzi wa jengo la PAPU, Mhandisi Hanington Kagiraki amesema kuwa jengo hili litakuwa na ghorofa 17 na ujenzi wake unagharamiwa kwa pamoja baina ya PAPU na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo hadi sasa kazi ya ujenzi na usimikaji wa nguzo za kujenga ghorofa 17 umefikia asilimiam 75 ambapo jumla ya nguzo 145 zimesikwa kati ya nguzo 192 zinazohitajika kujengwa na mradi huu ni wa kipindi cha siku 900 na umeanza mwezi Januari 2020 na utakamilika mwaka 2022.

Katibu Mkuu Msaidizi wa PAPU, Kolawole Aduloju amesema kuwa anaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano katika kujenga jengo hili na ujenzi unaendelea na wanaamini kuwa utakamalika kwa wakati

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mary Makondo amesema kuwa Serikali imenufaika kwa kupata ardhi ili mradi huu uweze kutekelezwa na hadi sasa vijana 70 wamepata ajira na tunatarajia watanzania na wana Arusha wataendelea kupara ajira

Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA MRADI WA MAJI SAME MWANGA KOROGWE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maji Maji wa Same – Mwanga – Korogwe wakati alipotembelea chanzo cha mradi huo eneo la la Nyumba yaMungu Wilaya ya Mwanga wakati akiwa ziarani mkoani Kilimanjaro tarehe 21 Machi 2024. Makamu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *