TANZANIA INATUHITAJI KULIKO TUNAVYOIHITAJI SISI.

#NiSisiSisi Watanzania

UZALENDO WA MH. JPM KWA NCHI YAKE 

Kwa muda mrefu wa Tanzania pamoja na wapinzani wa nchi yetu tulishawahi kupitia nyakati tofauti tofauti za kiuongozi, zikianzia kwa Baba wa Taifa Mzalendo hayati Mwl. Julius K. Nyerere,Mzee Ruksa A. Mwinyi, Mzee wa Uwazi na Ukweli B.W. Mkapa, Mzee wa Maisha Bora kwa Kila Mtanzania J. M. Kikwete na sasa tunaye Baba yetu na raia namba moja wa Nchi Yetu Ndugu.

Ad

John Pombe Joseph Magufuli.

Katika awamu zote hizi nne zilizopita kila mmoja kwa wakati wake walifanya yao kwa Taifa kwa kiasi ambacho walijitahidi pamoja na changamoto walizokuwa wanakutana nazo kwenye tawala zao.

Pamoja na awamu ya pili na awamu ya nne kufanya vema lakini tunaona kwa upana na kwa usubutu mkubwa kazi ambazo zilifanywa na awamu ya kwanza ya Baba wa Taifa Mwl. J. K. Nyerere kwa kujenga utengamano wa nchi na umoja wa kiTaifa pasipo kujari rangi zetu na makabila yetu mbali tukasimama kwenye uTanzania ulio wa pamoja.

Baada ya kazi kubwa hiyo iliyofanywa na Baba wa Taifa sasa tunaona tena Mawazo na Maono ya Baba wa Taifa yakiwa yamejitokeza kwenye awamu ya Tano ya Utawala wa Nchi yetu chini ya rais wetu mpendwa na raia namba moja wa Taifa kwa sasa Dr. John P. J.Magufuli

Uzalendo wake Mh. Dr. John.P.J.Magufuli uko wapi?

Tumeona kwa macho yetu na pasipo kuambiwa Mh. Rais akitenda mambo mengi ambayo kwa mwazo yalitoka awamu ya kwanza ya utawala wa nchi yetu na awamu zingine ziliyaweka kando kidogo na kilikuwa kilio cha waTanzania wengi pamoja na wapinzania na amekuja kuongezea mengine ambayo yanaendana na wakati huu na changamoto zake.

Kwa mfano wa kurejea tu Uzalendo wake unadhihirika hapa:

1. Kuthubutu kuhamishia Dodoma wizara zote.

Screen Shot 2018-09-01 at 1.11.32 PM.png

2. Kuanza ujenzi wa reli ya Umeme.

 

3. Kuziba mianya ya rushwa na ufisadi.

 

4. Kurejesha heshima na nidhamu makazini hasa kwa watumishi wa Umma.

5. Kurejesha watoto wa masikini kusoma bure toka shule za misingi mpaka sekondary kwa kutumia rasilimali zetu za ndani.

6. Kutokuwa na urafiki na wote wanaoenda kinyume na utaratibu wa kiutawala.

7. Kutengenza barabara za juu Dar.

8. Kuongeza mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ndani ya nchi.

9. Kusimamia ipasavyo ukusanyaji wa kodi na matumizi yake kuelekezwa kwenye mambo mhimu ya nchi.

10. Kufufua shirika letu la Ndege (ATCL) kwa kununua ndege mpya na sasa twapasua anga.

11. Kuimarisha ulinzi wa mipaka yetu.

12. Kuendelea kuongeza usafiri wa majini.

13. Kuendelea kwa ujenzi wa barabara za lami pamoja na kuunganisha mikoa na wilaya za nchi yetu.

14. Karejesha hadhi ya Urais (Akiwa ndio msemaji wa mwisho akiwa ndio raia namba moja wa Taifa)

15. Kaongeza usimamizi wa rasilimali zetu hasa madini.

NB

Haya ni machache kati ya yale mengi ambayo Mh. #JPM kaamua kwa dhati na pasipo kupepesa macho kuyasimamia kidete, kadhamira na anaonyesha njia kwa kila jambo ambalo anataka liwe ndio sifa ya uongozi.

Huu ni uzalendo wa rais wetu kwa nchi yake na wapinzani wetu walitamani siku nyingi Tanzania iwe na rais wa kufanya maamuzi na kuyasimamia,ndio huyu hapa JPM.

Walitamani rais ambaye haogopi kurejesha nidhamu makazini,ndio huyu hapa JPM.

Walitaka rais ambaye atafanya maamuzi magumu kwa ajiri ya kuwasaidia katika nyanja tofauti tofauti waTanzania, ndio huyu hapa JPM.

Walitamani tuwe na rais asiyekuwa na urafiki na mtu yeyote kwenye maswala ya uwajibikaji na utawala, huyu hapa JPM.

Huyu ndio mzalendo na najivunia kuwa na raia namba moja mwenye usubutu na mwenye kusimamia maamuzi yake.

Siku kadhaa zilizo pita kulikuwa na stofahamu ya makontena ya Mkuu wa Mkoa wa Dar ambayo yako bandalini na waTanzania walikuwa wanasubiria kauli ya Mkuu wa nchi, jana katoa msimamo wake kuwa lazima yalipiwe kodi la sivyo yapigwe mnada (Mh. Kaonyesha hana urafiki kwenye kazi)

Je! Watanzania tunataka rais mzalendo wa namna gani kwani kila vilio vya muda mrefu ndani ya nchi yetu vinashughulikiwa na hivi vimefanyika ndani ya miaka miwili na kidogo tu hata awamu yake ya kwanza hajamaliza.

Je! Mungu atupe nini waTanzania?

Hebu tushikane waTanzania tuwe na sauti ya pamoja huku tukisonga mbele kwa nia ya kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Tuendelee kuitikia Kauli mbiu ya Mh. Rais wetu mpendwa ‘HAPA KAZI TU’.

tusimame kidete kutetea Uzalendo unaoonyeshwa na Mh.Rais wetu kwa nia ya kutatua kero na changoto za maisha ya kila siku ya waTanzania wezetu katika nyanja tofauti tofuati ili tu kufikia Tanzania tunayoitamani kila wakati yenye fursa za kutosha.

Uzalendo ni vitendo na sio maneno na utu ni matendo kwani rais wetu kaonyesha njia na mwelekeo wa wapi Anataka twende na Tanzania yetu pasipo kuona haya.

Kutoka kwa: #RafikiWaMaendeleo

  • Mr Sheja Rb
  • Robert Shejamabu

 

Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS MAGUFULI AIPONGEZA MAHAKAMA NA WADAU KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Rais  Dkt. John  Magufuli ameipongeza Mahakama na wadau wake kwa hatua kubwa za kimaendeleo zilizopigwa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *