Hii ni moja ya barabra ambayo haikuwahi kujengwa kwa kiwango cha lami tangu nchi yetu ipate uhuru wake mwaka 1961. Awamu ya Tano ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaifanya katika kipindi cha miezi 30 pekee ambapo mwezi Aprili kwaka 2020 itakuwa imekamilia.

UJENZI WA BARABARA YA KIDATU – IFAKARA WASHIKA KASI

UJENZI WA MIUNDOMBINU (BARABARA YA KIDATU- IFA
Sehemu ya eneo lililoandaliwa kujengwa barabara ya Kidatu hadi Ifakara. Tayari mkandarasi yuko kazini kuendelea kusafisha eneo lote atalojenga barabara hiyo yenye urefu wa km 66.9 ambapo; Ujenzi huo unatarajiwa kuhusisha ujenzi wa Madaraja makubwa mawili, madaraja madogo Manne, Makalvati makubwa na madogo 271 na unatarajiwa kuwa na ubora wa kudumu kwa miaka 20.

 

  • Ni barabara yenye urefu wa km 66.9 ambayo haikuwahi kujengwa tangu Uhuru, ni  moja ya maamuzi ya Serikali ya Awamu ya Tano  baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kuamua kwa dhati kutekeleza kikamilifu ILANI ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 na ahadi zake wakati wa kampeni za urais.
RAIS MAGUFULI KATIKA UWEKAJI JIWE LA MSINGI KWENYE UJENZI WA BARABARA YA KIDATU - IFAKARA
Rais Magufuli akihutubia wananchi katika kijiji cha Nyandeo eneo la Kidatu mkoani Morogoro siku ya tarehe 05 Mei, 2018 kabla ya kuweka jiwe la msingi kuanzisha ujenzi wa barabara hii muhimu ambayo ikikamilika, itatengeneza historia na kuwa kipande muhimu katika ujenzi wa barabara kuu ya Morogoro-Mikumi – Ifakara kupitia daraja la Magufuli (kwenye Mto Kilombero)- Songea itakayorahisisha usafiri na usafirishaji kati ya eneo la Mikumi, Ifakara, Mhenge, Malinyi, Ulanga hadi Songea mkoani Ruvuma.
  • Mkandarasi tayari ameanza kazi haraka kama agizo la mheshimiwa Rais lilivyomtaka siku ya uwekaji jiwe la msingi wa ujenzi wa barabara hiyo
UJENZI WA BARABARA YA KIDATU - IFAKARA KWA KIWANGO CHA LAMIUNAENDELEA
Mkandarasi akiwa kazini na ujenzi wa barabara ya Kidatu – Ifakara (kiwango cha lami) unaendelea kwa kasi ambapo ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili 2020.
  • Usafishaji wa eneo itakapojengwa barabara hiyo unaendelea na kilometa nyingi zikisafishwa.
ujenzi wa barabara ya Kidatu hadi Ifa
Ujenzi wa barabara hii, pia utahusisha ujenzi wa daraja jipya katika eneo la Ruaha ambapo litajengwa daraja kubwa la Great Ruaha lenye urefu wa mita 130

 

Ujenzi wa barabara hii ya Kidatu – Ifakara kwa kiwango cha lami, unatarajiwa kujengwa kwa miezi 30 na utagharimu kiasi cha Tsh. Bilioni 111.4 na unafadhiliwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (European Union), Shirika la Misaada la Uingereza (UK Aid) na Shirika la Misaada la Marekani (USAID).

UZINDUZI WA UJENZI WA BARABARA YA KIDATU - IFAKARA TAREHE 05/05/2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kukata utepe baada ya kufungua kitambaa kuashiria kuwekwa jiwe la msingi pamoja na viongozi wengine wakiwemo Mwakilishi wa DFID nchini Beth Arthy aliyeshika mkasi pamoja na Mhe. Raos wakiwa sambamaba na Mkuu wa Umoja wa Jumuiya ya Ulaya Balozi Roeland van de Geer pamoja, Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na wabunge mbalimbali wa mkoa wa Morogoro.
Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA KATIBU MTENDAJI SADC, BALOZI WA EU NA BALOZI WA CHINA

Rais Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 05 Februari, 2020 amekutana na Katibu Mtendaji wa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *