WAZIRI KALEMANI AKAGUA REA III WILAYANI,BUHIGWE NA KIGOMA VIJIJINI

  • Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Kasulu, Kigoma Vijijini na Buhigwe mkoani Kigoma kwa lengo la kukagua mradi wa usambazaji umeme vijijini wa Awamu ya Tatu (REA III) ambapo pia aliwasha  umeme katika baadhi ya Vijiji.
  • Akiwa wilayani Kasulu, Dkt Kalemani alikagua kazi zinazofanywa na mkandarasi katika Kijiji cha Ruhita ambapo alikuta Kijiji hicho bado hakijaunganishwa umeme na kumuagiza Mkandarasi, kampuni ya CCCE Etern kufikisha umeme kijijini hapo baada ya siku 15.
  • Aidha, alimtaka Meneja wa TANESCO, Wilaya ya Kasulu kuhakikisha kuwa, anasimamia suala ya uchoraji wa ramani za kuingiza umeme ndani ya nyumba za wananchi kwani kuna baadhi ya watu binafsi wanaofanya kazi hizo wamekuwa wakiwatoza wananchi gharama kubwa bila kujali tofauti ya ukubwa au udogo wa kazi.
  • Vilevile, Dkt Kalemani alimtaka Meneja huyo kuhakikisha kuwa watu wanaofanya kazi za kufunga nyaya za umeme ndani ya nyumba za wananchi wanatambulika na TANESCO ili kuepusha utapeli na kufanya kazi chini ya viwango vinavyotakiwa.
WANANCHI
Wananchi katika Kijiji cha Bulimanyi wilayani Buhigwe, Mkoa wa Kigoma wakimsikiliza Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani (hayupo pichani) wakati alipofika kijijini hapo kukagua miundombinu ya usambazaji umeme.
  • Awali Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Simon Anange alimweleza Dkt Kalemani kuwa, wananchi wa Kijiji hicho wamesubiri umeme kwa muda mrefu baada ya kupata ahadi ya kupelekewa nishati hiyo, hivyo wanaomba Mkandarasi akamilishe kazi hiyo mapema ili waweze kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo za kiuchumi.
  • Akizungumzia suala hilo, Dkt Kalemani alisema kuwa, Mkandarasi ambaye ni kampuni ya CCCE Etern ameanza kazi mwezi Januari mwaka huu tofauti na wanandarasi wa umeme katika maeneo mengine nchini ambao walianza kazi mwaka jana, hii ni kwa sababu ya masuala ya kisheria yaliyojitokeza hapo awali lakini sasa Mkandarasi huyo anaendelea na kazi.
  • Akiwa wilayani Buhigwe, Dkt  Kalemani alikagua miundombinu ya umeme katika Kijiji cha Bulimanyi ambacho tayari kimeshafikishiwa  umeme na kaya zaidi ya Kumi zimeshaunganishwa na nishati hiyo na kumuagiza Mkandarasi kupeleka umeme katika Vijiji vyote vya Wilaya hiyo.
  • Dkt. Kalemani pia alikagua miundombinu ya umeme katika Kijiji cha Mkigo wilayani Kigoma Vijijini, ambapo pamoja na kuzungumza na wananchi, aliwasha umeme katika Kijiji hicho.
Ad

Unaweza kuangalia pia

UUNGANISHAJI UMEME VIJIJINI UENDE SAMBAMBA NA IDADI KUBWA YA KUWAWASHIA WATEJA

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, amewaagiza Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini(REA) pamoja …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *