Nchi yetu imefanikiwa katika nyanja mbali mbali kukuza uchumu imara na madhubuti kwa Watanzania wote. Baadhi ya mafanikio ni haya katika picha hii.

MABENKI YETU, SASA TAMBUENI MADINI KAMA DHAMANA KWA WACHIMBAJI WADOGO WADOGO – WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa alipokuwa akihutubia wakazi wa Geita katika hafla ya kufunga maonesho ya madini mkoani humo.

“Mabenki yetu anzisheni utaratibu wa kuweka.. dhamana, kuweka madini ya wananchi.. nunueni dhahabu. Nunueni dhahabu; Ili hawa wananchi badala ya kuhangaika kwenda kwenye minada amabapo wanalaliwa laliwa, aende benki ahifadhi kule.” – Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa

“Badala ya kuleta fedha eweke madini yake.. atakuja kuyachukua mwakani nayo yatakuwa yameongezeka thamani. Kwahiyo nitoe wito kwa mabenki badilikeni! Pokeeni madini azisheni hicho kitengo cha kupokea madini dhahabu, wekeni..” – Mhe. Waziri Mkuu

Ad
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,akionyesha zawadi aliyopewa kwenye maonesho ya madini akiwa na Waziri wa Madini Bi. Angela Kairuki katika hafla ya kufunga maonesho hayo mkoani Geita

“Kwahiyo Mkurugenzi Mkuu Benki Kuu; Pamoja na maelezo yote hayo, kaa na mabenki yako ya biashara.. kaeni anzisheni utaratibu wa kupokea dhahabu kwenye benki ili wachimbaji wadogo akichimba akipata gramu zake tatu – nne, akimbize benki kwenda kuweka pale kama fedha.. badala ya fedha anaweka madini yake. Siku ya siku akija, akiona bei nzuri.. anakuja anachukua hela kwa thamani hiyo.” – Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu Mhe. kassim Majaliwa akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Eng. Robert Gabriel baada ya kuwasili mkoani Geita
Ad

Unaweza kuangalia pia

WAZIRI MKUU AMPONGEZA BONDIA SALIM MTANGO ALIYESHINDA MKANDA WA DUNIA WA UBO

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *