JESHI LA POLISI LIJITAFAKARI KWA BAADHI YA MATENDO YAKE – RAIS MAGUFULI

  • Rais  Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 04 Machi, 2019 amewaapisha Mawaziri 2, Balozi 1 na kushuhudia Naibu Makamishna wa Polisi 5 wakivishwa vyeo vipya vya Kamishna wa Polisi (CP) na kuapishwa kuongoza Kamisheni za Polisi.
RAIS-MAGU-2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi katika picha ya pamoja na Makamishna watano kutoka jeshi la Polisi, Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Palamagamba Kabudi, pamoja na Balozi Yahya Simba mara baada ya hafla ya Uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Mhe. Balozi Dkt. Augustine Phillip Mahiga kuwa Waziri wa Katiba na Sheria na Mhe. Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
  • Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Mhe. Hassan Simba Yahya kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zambia. Mhe. Balozi Simba amechukua nafasi ya Mhe. Balozi Abdulrahman Kaniki ambaye amemaliza muda wake.
RAIS MAGUFULI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Dkt. Augustine Mahiga kuwa Waziri wa Katiba na Sheria Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameshuhudia Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Simon Sirro akiwavisha cheo cha Kamishna wa Polisi na kuwaapisha, Naibu Makamishna wa Polisi 5.
  • Walioapishwa ni CP – Charles Omari Mkumbo ambaye ameteuliwa kuwa Kamishna wa Intelijensia ya Jinai, CP – Liberatus Materu Sabas aliyeteuliwa kuwa Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, CP – Shabani Mrai Hiki aliyeteuliwa kuwa Kamishna wa Maabara ya Uchunguzi wa Kisayansi, CP – Leonard Paul Lwabuzala aliyeteuliwa kuwa Kamishna wa Fedha na Lojistiki na CP – Benedict Michael Wakulyamba aliyeteuliwa kuwa Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Utumishi.
  • Akizungumza katika tukio hilo Mhe. Rais Magufuli amewapongeza Mawaziri, Balozi na Makamishna wa Polisi kwa kuteuliwa kwao na amewataka kwenda kutekeleza majukumu yao vizuri  ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko ya kuondoa dosari zilizopo katika maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi zaidi huku wakiweka mbele maslahi ya Taifa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • Mhe. Rais Magufuli amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kazi nzuri linayoifanya lakini ametaka lijitafakari juu ya baadhi ya matukio ambayo yanaacha maswali mengi kwa wananchi juu ya hatua zinazochukuliwa na polisi, na ametolea mfano wa tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji, vitendo vya rushwa, Polisi kuhusishwa na magendo, vitendo vya rushwa na dawa za kulevya, pamoja na hatua zinazochukuliwa dhidi ya Maafisa wa Polisi wanaoshindwa kufanya kazi kwa tija.
Screen Shot 2019-03-04 at 18.16.05
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Yahya Simba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zambia Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • Mhe. Rais Magufuli amemtaka IGP – Simon Sirro kutosita kuwaondoa Maafisa wa Polisi wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kuteua ama kupendekeza Maafisa wapya wenye uwezo wa kufanya kazi vizuri, na pia ametaka Polisi iondokane na utamaduni wa kuwapeleka Makao Makuu ya Polisi Maafisa ambao wanashindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwenye vituo vya kazi wanavyopangiwa.
RAIS MAGUFULI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Dini mara baada ya hafla ya Uapisho Ikulu jijini Dar es Salaa.
  • Hafla ya kuapishwa kwa Mawaziri, Balozi na Makamishna wa Polisi imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Mawaziri na Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu, Viongozi Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Madhehebu ya Dini na Majaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani.
RAIS MAGUFULI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi katika picha ya pamoja na Maofisa Mbalimbali wa Jeshi kutoka Jeshi la Polisi mara baada ya hafla ya Uapisho wa viongozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam.
  • Viongozi walioapishwa pia wamekula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Mstaafu Harold Nsekela.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Ad

Dar es Salaam

04 Machi, 2019

Ad

Unaweza kuangalia pia

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE DKT. NDUMBARO AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WA NCHI TANO HAPA NCHINI

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *