MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KUFUNGUA MAONYESHO YA NANE MKOANI SIMIYU

Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Bwana Gerald Kusaya mapema tarehe 29 Julai, 2020 ametembelea Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu na baadae alielekea katika Viwanja vya Nyakabindi.

Katibu Mkuu Kusaya aliekea katika Viwanja vya Nyakabindi ili kujionea na kukagua maandalizi ya eneo la maonyesho ikiwa ni pamoja na kujionea jengo la Wizara ya Kilimo ambalo litakuwa sehemu ya kutolea mafunzo ya kudumu kwa Wakulima wa Mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara.

Ad

Awali katika mazungumzo yake na Mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Bwana Ekwabi Mujungu amemweleza Katibu Mkuu Kusaya kuwa maandalizi kwa upande wa mkoa wa Simiyu na Halmashauri zake yanaendelea vizuri.

“Tarehe 1 Agosti, 2020 tunataraji; Mgeni wetu Rasmi; atakuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ambaye atafungua rasmi Maadhimisho ya mwaka huu na baadae Rais wa Awamu ya Tano, Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli atahitimisha; Nawakaribisha Wananchi wote.” Katibu Mkuu Kusaya

Ad

Unaweza kuangalia pia

Mitazamo ya Uongozi ya Mhe. Ummy Ally Mwalimu katika Sekta za Afya, Maendeleo ya Jamii, na Haki za Watoto

Ummy Ally Mwalimu ameonyesha mitazamo ya uongozi yenye mwelekeo wa kujali maendeleo na ustawi katika …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *