Mshindi wa Tuzo za Sinema Zetu kipengele cha muigizaji Bora wa Kike mwaka 2019

MAISHA HALISI YA MSHINDI WA TUZO SINEMA ZETU (SZIFF 2019), MUIGIZAJI BORA WA KIKE; Ni funzo chanyA+

• Anaitwa Flora Kihombo binti mwenye umri wa miaka 10 anayeendelea na elimu ya msingi (Darasa la Sita)

MSHINDI 2.jpg
Flora Kihombo (10) ambaye aliigiza katika filamu ya Kesho na kufanikiwa kuingia katika kinyang’anyilo cha kuwania tuzo ya muigizaji Bora wa kike mwaka 2019, alifanikiwa kuwashinda waigozaji mahiri nchini.

•• Ni mtoto wa nne kuzaliwa katika familia duni yenye watoto 7 ambapo kutokana na ugumu wa maisha, wazazi wake iliwalazimu muwandikisha kwenye kituo cha kulea watoto wanaoishi katika mazingira magumu mwaka 2015 ili apate fursa ya kutimiza ndoto zake za kuwa muingizaji bora na daktari bingwa wa macho.

Ad

••• Asimulia hali halisi ya nyumbani kwao ambapo hula mlo mmoja pekee(ugali na mboga za majani) katika kipindi chote cha ukuaji wake

•••• Atokwa na machozi baada ya kuulizwa swali kuhusu nyumba ya familia yao. Asema ilibomoka kwa mvua kali mwaka jana 2018 na toka wakati huo mpaka sasa familia imejihifadhi kanisani.

••••• Asema fedha alizozipata baada ya kutwaa Tuzo ya Muingizaji Bora wa Kike – SZIFF 2019, atazitumia kujenga nyumba ya kuishi familia yake sambamba na kununua mahitaji ya nyumbani kama chakula na nguo kwaajili ya baba na mama yake.

•••••• Inafaa kutafakari na kujifunza; Sisi si wastahili zaidi ya wengine

maana #SisiNiTanzaniaMpyA+

Fuatilia mahojiano mafupi yaliyofanywa mara baada ya kumalizika kwa hafla ya utoaji tuzo hizo usiku wa kuamikia Februari 23, 2019.

Ad

Unaweza kuangalia pia

SERIKALI KUENDELEA KUCHUKUA HATUA KWA WAZALISHAJI NA WASAMBAZAJI WA MIFUKO ISIYOKIDHI VIWANGO – WAZIRI ZUNGU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *