SOKO LA UNUNUZI NA UUZAJI MADINI MKOA WA KATAVI, LAZIDI KUIMARIKA

  • Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera amefanya ziara katika  mgodi wa Dilifu wa wachimbaji wadogo na mgodi mkubwa wa Katavi, Kapufi mining.
  • Akizungumza katika ziara hiyo mkuu wa Mkoa amewaasa wachimbaji kutumie soko ya madini lilolifunguliwa mkoani humo kuuza madini yao
WACHIMBAJI
Baadhi ya Wachimbaji Mkoani Katavi wakimfatilia Mkuu wa mkoa,(hayupo pichani) wakati alipofika kuzungumza na wachimbaji hao.
  • Homera ameahidi  kupambana na watoroshaji wa madini ya dhahabu na mpaka sasa wamekamata watu wawili  kwa kununua dhahabu kinyume cha sheria kwa wakazi wa Mkoani Katavi.
  • Hata hivyo Mkuu wa Mkoa Homera amesema kuwa  soko la madini limeshafanya biashara kwa kununua dhahabu gramu 238, May 23/2019,na kuongeza  kuwa  jambo hilo lilimfanya aanze kufatilia na  kubaini kuwa  dhahabu nyingi inayopatikana Mkoani Katavi inauzwa nje ya mkoa wa Katavi nakupelekea soko hilo kusuasua na kuamua  kuyafanyia kazi mapungufu ya soko hilo ili kudhibiti dhahabu kuuzwa bila kufata utaratibu.
HO 3-01
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera akiwa katika moja wa mgodi mkoani humo.
  • ”Mpaka sasa soko  linaridhisha na kufuatia oparesheni mbalimbali zinazoendelea Soko linaendelea kufanya kazi ya ununuzi na uuzaji wa madini na mpaka sasa gramu 6317.2 sawa na Kg 6 na Grams 317.2 yenye thamani ya shilingi milioni 519,155,127.56 zimenunuliwa kwa kipindi cha Mei na Juni 30/2019 na serikali kupata mrahaba (Royality7%) shilingi  milioni 36,340,858.92 na Service levy 0.3 Tsh.milioni 1,401,718.85” alisema Homera
  • Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kuwa wanaendelea kuimarisha mifumo ya kibenki  katika soko hilo na kuendelea kuwabana  madalali na wanunuzi wenye leseni na wachimbaji mbalimbali ili kuhakikisha  wanauza madini yao kwenye soko la mkoa huo.
Ad

Unaweza kuangalia pia

MADINI NA VIWANDA VYALETA MAGEUZI YA UCHUMI NCHINI

Mauzo ya bidhaa nje ya nchi zisizo kuwa za kawaida yameongezeka kwa asilimia 41.9 kwa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *