Maktaba ya Mwezi: August 2020

RAIS MAGUFULI AKAGUA MAGARI YALIYOTAIFISHWA NA AAGIZA YAGAWANYWE SERIKALINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Agosti, 2020 amekagua magari yaliyotaifishwa baada ya kuhusika katika matukio ya uhujumu uchumi, na kisha kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani Jijini Dodoma. Sehemu ya magari makubwa na madogo 130 yaliyotaifishwabaada ya kuhusika katika …

Soma zaidi »

WANANCHI WAUSIWA KUTUNZA AMANI WAKATI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI NA SIO KUVUNJA UDUGU

Wananchi Mkoani Rukwa wameusiwa kuendelea kuitunza amani katika kipindi chote cha kampeni wakati tukielekea kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika siku ya Jumatano tarehe 28.10.2020 utakaowapa nafasi ya kuwachagua Madiwani katika ngazi za Kata, Wabunge katika ngazi za Majimbo pamoja na kumchagua Rais wa nchi ya Tanzania.  Usia huo umetolewa na Mkuu …

Soma zaidi »

WAZIRI MHAGAMA AIASA JAMII KUTOPUUZA VYAKULA VYA ASILI

NA.MWANDISHI WETU Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ameiasa jamii kuendelea kutumia vyakula vya asili ili kuwa na afya bora na kuondokana na magonjwa yatokanayo na lishe duni. Ameyasema hayo wakati wa ziara yake …

Soma zaidi »

WATENDAJI WA MIKOA WAHIMIZWA KUSIMAMIA USTAWI WA SEKTA YA FEDHA NCHINI

Na Farida Ramadhani, WFM, Morogoro Serikali imewataka watendaji wa mikoa kuhakikisha wanasimamia na kuendeleza Sekta Ndogo ya Fedha nchini kwa kuhamasisha watoa huduma katika sekta hiyo wanasajiliwa na kukata leseni kwa mujibu wa Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018. Agizo hilo limetolewa na Kamishna wa Idara ya …

Soma zaidi »

NAIBU KATIBU MKUU NISHATI AKAGUA MAENDELEO UJENZI WA MRADI WA UMEME WA JULIUS NYERERE (JNHPP)

Mafundi wakiendelea na kazi ya kukamilisha lango la handaki la kuchepusha maji ya mto wakati wa kujenga Bwawa la kuzalisha umeme kwa kutumia maporomoko ya maji ya Bonde la mto Rufiji wa Julius Nyerere. Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Mhandisi Leonard Masanja alifanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi …

Soma zaidi »

TIC YAFANIKISHA MPANGO WA KAMPUNI YA MISRI KUWEKEZA KIWANDA CHA VIFAA VYA UMEME TANZANIA

Na Mwandishi Wetu Dar es Salaam Mwakilishi wa Kampuni ya kuzalisha vifaa vya umeme ya Elsewedy Electric ambaye ni Mkurugenzi Mkaazi wa Afrika Mashariki wa Kampuni hiyo injinia Ibrahim Qamar kutoka nchini Misri anayewekeza nchini Tanzania amesema kuimarika kwa Sera, Sheria na mazingira mazuri ya Uwekezaji Nchini Tanzania ikiwa ni …

Soma zaidi »

RAIS MAGUFULI AZINDUA KANISA NA AFANYA HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI WA MSIKITI CHAMWINO, DODOMA

Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Imakulata Ikulu Chamwino leo Jumapili Agosti 23,. 2020 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiombewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya aliposhiririki Misa Takatifu ya Dominika ya 21 ya Mwaka “A” na kuzindua Kanisa, …

Soma zaidi »

TAASISI YA MOYO (JKCI) YAPOKEA MASHINE YA KUPIMA UMEME WA MOYO

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimpulizia kisafisha mikono (hand sanitizer ) Daktari bingwa wa magonjwa ya watoto Antke Zuechner wa Jamii ya Ujerumani kwa magonjwa ya watoto ya Ukanda (Germany Society for tropical pediatrics) mara baada ya kumkabidhi msaada wa mashine ya kupima …

Soma zaidi »

MRADI WA PERI URBAN KUKAMILIKA KWA WAKATI

Hafsa Omar-Dodoma Naibu katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Leonard Masanja amewataka wakandarasi wanaotekeleza mradi wa Umeme katika Vijiji vilivyo pembezoni mwa Mji (Peri-Urban) kukamilisha utekelezaji wa miradi yao ndani ya muda uliopangwa. Ameyasema hayo,Agosti 19,2020,wakati alipokuwa kwenye kikao na  Wakandarasi  wa mradi wa Per-Urban, kilichofanyika katika ofisi za Wizara …

Soma zaidi »